.
25th October, 2021
Mzozo wa uongozi katika kaunti ya Nairobi unaendelea kutokota baada ya mahakama ya juu zaidi kusitisha hafla ya kumuapisha Ann Kananu kama Gavana wa Nairobi. Uamuzi huo umechukuliwa baada ya gavana wa zamani Mike Sonko kuwasilisha rufaa mbele ya mahakama hiyo akipinga uamuzi wa mahakama ya rufaa uliotoa kibali kwa kananu kuapishwa.