8th May, 2021
Msichana mmoja kutoka eneo la Webuye kaunti ya Bungoma aliyemaliza kidato cha nne anaishi na risasi mbili mwilini baada ya kupigwa risasi na mwanafunzi mwenza miaka minne iliyopita alipokuwa anasoma shule ya upili ya Lokichogio katika kaunti ya Turkana. Phanice Weyaga amesalia kuvumilia maumivu akimshukuru mungu kwa kuponea kifo.