.
14th April, 2021
kijiji cha shirulo katika eneo la ikolomani kaunti ya kakamega kimegutushwa na vile vile kukumbwa na furaha tele baada ya jamaa mmoja aliyedhaniwa kuaga dunia na hata kuzikwa mwaka jana kujitokeza hii leo. antony muhati mwenye umri wa miaka 58 na ambaye hufanya kazi za kibarua kitale anasema alisikia taarifa kuhusu kifo chake ndiposa akarejea. familia sasa inasema italazimika kumfanyia matambiko na kufukua mwili uliozikwa ili kuurejesha katika makafani ya kitale.