.
26th January, 2021
Wenyeji wa mtaa wa Buxton kaunti ya Mombasa wana hadi mwezi machi mwaka huu kufahamu iwapo nyumba zao zitabomolewa ili kutoa nafasi ya ujenzi wa nyumba kisasa.
Mradi huo unaoendeshwa na serikali ya kaunti ya Mombasa pamoja na kampuni ya nyumba ya Buxton point inalenga kubomoa nyumba 520 na kujenga nyumba zingine 1500. Wenyeji waliwasilisha ombi mahakamani wakitaka ilani ya kusimamisha ubomoaji huu wakidai mradi huo wa kima cha shilingi bilioni 6 sio halali na madhumuni yake ni kuwanyan'ganya ardhi hiyo ya ekari 14.