26th January, 2021
Mmojawapo wa washukiwa wa mauaji huko Kiambu Sarah Muthoni, sasa ameachiliwa na mahakama baada ya kufanywa shahidi. Hata hivyo kesi dhidi ya mshukiwa mkuu Lawrence Warunge haijaendelea baada ya ripoti ya uchunguzi wa akili kubaini bado hana uwezo wa kuendelea na kesi hiyo. Sasa Warunge atasalia rumande huku akipata matibabu ya akili kwa siku thelathini.