26th January, 2021
Shule nne kwenye mpaka wa kaunti za Baringo na Turkana zimefungwa kufuatia utovu wa usalama katika eneo la Kapedo. Na baada ya serikali kutangaza kwamba masomo katika maeneo hayo yamesitishwa hadi usalama urejee, hali hiyo sasa imewaacha wanafunzi wengi hasa watahiniwa kutoka Kapedo na maeneo mengine yanayoandamwa na hali tete ya usalama kwenye njia panda.