.
31st October, 2020
Wakenya sasa watapokea huduma bora ya afya bila malipo iwapo mpango wa serikali wa kueneza mradi wa uhc nchini kote utafaulu. rais uhuru kenyatta amesema kuwa ni azma ya serikali yake kupunguza gharama za huduma ya afya na kuboresha huduma hizo. mradi wa uhc ulifanyiwa majaribio katika kaunti nne za kisumu, machakos, nyeri na isiolo, na kulingana na rais, ulikuwa wenye mafanikio makubwa. lakini kama anavyoarifu ibrahim karanja, huenda mradi huo ukakumbwa na tishio la kufeli haswa katika wizara iliyojaa visa vya ubadhirifu wa fedha.