21st October, 2020
Hisia mbali mbali zinazidi kutolewa na viongozi baada ya ripoti ya BBI kuzinduliwa rasmi mapema leo. Gavana wa kaunti ya Meru Kiraitu Murungi ameunga mkono ripoti hiyo na kusema kuwa imegusia suala la fedha zinazogawiwa kaunti kwa kuongeza kutoka asilimia 15 hadi asilimia 35. Kiraitu ambaye amepigia debe kuongezwa kwa fedha kwa kaunti amesema kuwa wakazi wa meru na viongozi hawataiunga mkono ripoti hiyo kipofu tu, bali wataisoma kabla ya kutoa msimamo wa pamoja. Ameongeza kuwa patakuwepo na mkutano mkubwa katika siku zijazo utakaohusisha wadau mbali mbali wakiwemo viongozi na wananchi kutoka kaunti ya Meru.