×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Takwimu za Korona: Visa 148 vipya vyaripotiwa leo huku watu 4 wakifariki

18th September, 2020

Watu wengine wanne wamefariki katika muda wa saa 24  zilizopita kutokana na makali ya virusi vya korona huku maambukizi mapya 148 yakirekodiwa hii leo. idadi ya vifo sasa ni watu 646 na maambukizi 36, 724.miongoni mwa walioambukizwa 145 ni wakenya na watatu ni raia wa kigeni.umri wa waathiriwa ni kati ya miaka 2 na 75.kaunti ya mombasa ndio imerekodi visa vingi ikifuatwa na nairobi.kaunti nyengine ambazo zimeandikisha maambukizi mapya ni laikipia, kiambu, nakuru,embu, uasin gishu, kajiado, taita taveta, kisumu. Kitui, trans nzoia, baringo, elgeyo marakwet, kwale, machakos, kericho, makueni na muranga.habari njema ni kuwa watu wengine 98 wamepona na kuruhusiwa kwenda nyumbani na kufikisha idadi ya waliopona hadi watu 23,709.

 

.
RELATED VIDEOS