9th April, 2021
Sasa ni wazi kwamba huenda naibu wa rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanafanya majadiliano ya kushirikiana kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao. Haya yamejitokeza baada gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya kukutana na Raila Odinga kwa mkutano wa saa tano kuanzia saa tatu asubuhi, siku moja tu baada ya kukutana na William Ruto katika mbuga ya wanyama pori ya Maasai Mara.