9th April, 2021
Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini cotu Francis Atwoli amechaguliwa tena kama katibu mkuu wa muungano huo kwa kipindi kingine cha miaka mitano... Atwoli alichaguliwa tena hii leo kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa tom mboya kaunti ya kisumu... Akizungumza baada ya uchaguzi huo atwoli ameishauri serikali kutumia fedha inazokopa kuwapiga jeki wannachi wanaojihusisha na biashara haswa katika kipindi hiki kigumu cha janga la korona ambapo biashara nyingi zimeathirika, na kuwalazimisha wananchi wengi kuzifunga.