9th April, 2021
Mumewe malkia Elizabeth mfalme Phillip amefariki akiwa na miaka 99. Kulingana na msemaji wa familia yao huko Buckingham, marehemu aliaga dunia katika makazi yao ya kasri la windsor. Malkia elizabeth aliolewa na mumewe mnamo mwaka 1947, miaka mitano kabla ya kutawazwa malkia na alikua malme aliyehudumu kwa mda mrefu katika historia ya uingereza. Kwa hafla nyingi za umma ama kitaifa malkia elizabeth aliandamana na mumewe sako kwa bako na ufalme huo unachukuliwa kwa uzito wa hali ya juu na serikali ya uingereza. Familia ya mwanamflame philip na malkia elizabeth ilijaaliwa watoto 4, wajukuu 8 na vitukuu 10.
Kulingana na taarifa kutoka kasri la buckingham, ilieleza kuwa marehemu alifariki mapema asubuhi, taarifa iliotolewa na malkia elizabeth...