9th April, 2021
Mahakama ya kibera imemuagiza binti ya mfanyibiashara na mwanasiasa maarufu nchini kusalia korokoroni hadi shahidi mkuu katika kesi ya biashara ya ngono atakapotoa ushahidi wake. Hakimu mkuu wa mahakama hio Esther Bhoke alitoa amri hizo baada ya kutupilia mbali ombi la kuachiliwa kwa dhamana la faith bwibo, ambaye ni mwnafunzi wa chuo kikuu na mshtakiwa mwenza abdirazak adan. Mahakama na upande wa mashtaka ulikubaliana kutowaachilia kwa dhamana kwa kuwa kuna uwezekano wa kuharibu ushahidi. Hakimu bhoke alisema kesi hio ina uzito mkubwa kwa wawili hao, uhalifu ulioteklezwa katika mtaa wa mugiya south c mnamo tarehe20 mwezi machi. Kesi hio itatajwa tarehe 20 mwezi huu wa aprili.