19th February, 2021
Seneta wa Baringo Gideon Moi ametangaza ujenzi wa mabarabara na miradi zingine mbalimbali za serikali, katika kaunti ya Baringo, akizungumza katika mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa benki ya cooperative na mwandani wa hayati rais Moi, Hosea Mundui Kiplagat, Gideon ameahidi kushirikiana na rais Uhuru Kenyatta, kuhakikisha kuwa miradi iliyoahidiwa imekamilika. Aidha katika mazishi hayo, wito ulitolewa kwa naibu wa rais William Ruto kushirikiana na Gideon, ili kuunganisha jamii.