19th February, 2021
Baada ya kukaa mwaka mmoja bila kuandaa hafla la kusherekea wana skauti nchini, shirika la wana skauti wamerejea kwa kishindo wakianda hafla ya wanaskauti itakayoandaliwa katika kaunti ya nyeri hapo kesho wanaskauti wamejihusisha na miradi kusaidia shule za eneo hili ikiwemo kutoa mabati na kupaka rangi kwenye darasa za shule eneo hili ikiwa moja wapo ya njia za wanaskauti kusaidia jamii kwa kubadilisha maisha. Haya yanajiri huku shirika likitangaza kuwa wataanza upya kuwapiga msasa wanakamati kwenye shirika hilo wakidai kuwa kuna baadhi ya watu wanaoendeleza shughuli za wana skauti bila idhini yao.