19th February, 2021
Chama cha walimu wa sekondari na vyuo, kuppet, sasa kinaitaka taasisi ya kukuza mitaala nchini, kicd, kuandaa mwongozo wa kuwaelekeza wazazi kuhusu majukumu yao kwenye mtaala wa cbc. Katibu mkuu, akello misori, amesema kutokana na hali kwamba wazazi ni kiungo muhimu katika elimu ya watoto kwenye mtaala huo mpya wa elimu, itakuwa bora kwa kicd kuwahamasisha wazazi na walezi kuhusu majukumu yao.