×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

KNQA yawaonya wakenya wajanja wanaotumia vyeti bandia

19th February, 2021

Serikali imetoa tahadhari kwa wakenya walioajiriwa kupitia vyeti ghushi vya elimu kuwa wataandamwa na kukabiliwa kwa mujibu wa sheria. Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya taifa ya kutathmini na kuainisha hitimu, KNQA, dkt Juma Mukhwana, amesema tayari mamlaka hiyo imeishirikisha idara ya ujasusi, DCI, tume huru ya uchaguzi na uratibu wa mipaka, IEBC, na ile ya maadili na kupambana na ufisadi, EACC, ili kuwanasa wahusika. Aidha dkt mukhwana ameonya kwamba huenda watakaopatikana na hatia wakashtakiwa na kuagizwa warejeshe mishahara yote waliyopokea walipokuwa kwenye ajira.

 

.
RELATED VIDEOS