19th February, 2021
Rais Uhuru Kenyatta ameendelea kupigia debe mswada wa marekebisho ya katiba wa BBI kwenye ziara zake vitongojini Nairobi. Rais Kenyatta amesema mapendekezo kama kuongezwa kwa sehemu za uwakilishi ni njia ya kuongeza fedha mashinani. Rais pia ametia msisitizo kwa siasa bila fujo na umuhimu wa maendeleo. Alizungumza kwenye uzinduzi wa vituoa vya tekaji maji na hospitali mbili moja eneo la Soweto, Kayole na nyingine eneo la ushirika, Dandora.