7th May, 2021
Hospitali ya misheni Tenwek katika wiki moja ijayo itatoa huduma bila malipo kwa kwa kina mama wote kusherehekea siku ya dunia ya kina mama. Akizungumza baada ya kupokea msaada wa vifaa vinavyotumika nyumbani kutoka katika kampuni ya bidco africa afisa mkuu mtendaji wa hospitali hiyo ya Tenwek Shem Tangus amesema kuwa wanatambua umuhimu wanawake nchini. Miongoni mwa huduma watakazopata ni pamoja na kuwapima kina mama saratani ya matiti na kutoa huduma za ushauri nasaha. Mwakilishi wa Bidco Lawrence John amesema wamefanya kuonyesha jinsi wanavyojali afya ya kina mama