7th May, 2021
Pameibuka maswali mengi kuliko majibu kuhusu utendakazi wa maafisa wa polisi katika vituo vya polisi vya Kiptagich na Olenguruone, katika eneo bunge la Kuresoi kusini kaunti ya Nakuru. Maafisa katika vituo hivi viwili, wameelekezewa vidole vya lawama kwa madai ya kutumia nguvu kupita kiasi wanapotengamana na raia, jambo ambalo limesababisha vifo vya watu huku wengine wakijeruhiwa mwilini na pia kisaikolojia. Ibrahim Karanja anaelezea kuhusu hali hii, ambayo kwa kipindi cha juma moja lililopita limesababisha vifo cha watu wawili.