7th May, 2021
Waziri wa elimu, Profesa George Magoha, ametangaza kwamba ufunguzi wa shule utafanyika jumatatu ijayo, Mei tarehe kumi, jinsi ilivyoratibiwa. Akizungumza katika shule ya sekondari ya starehe baada ya kukamilika rasmi kwa usahihishaji wa mtihani wa kcse, Waziri Magoha aliongeza kwamba serikali imo mbioni kuhakikisha kwamba walimu wote wanapokea chanjo ya korona kufikia mwishoni mwa mwezi huu.