.
29th November, 2021
Wafungwa watatu waliotoroka jela ya Kamiti, na kutiwa mbaroni eneo la Kitui siku tatu baadaye, wamefungwa kifungo cha miezi kumi na mitano baada ya kukiri kosa la kutoroka jela.
Watatu hao pamoja na mfungwa mwengine anayedaiwa kuwasaidia kutoroka walifikishwa katika mahakama ya kahawa.
Wafungwa hao wameomba wasirudishe katika jela ya Kamiti na wamedai kuwa wapo baadhi ya maafisa wa jela waliowasaidia kutoroka na bado wako huru.