Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza Tony Blair amesita kuwa mjumbe wa Umoja wa Mataifa Mashariki ya Kati. Kuangazia muda wake akiwa mjumbe, itabainika wazi kwamba hakufanikisha lolote katika mzozo huo. Wakosoaji wake wanasema amejiweka karibu sana na serikali ya Israel na hawezi kuwajibika kutetea masilahi ya Wapalestina.
Kwa upande mwingine, wadadisi wanaelewa kwamba jukumu la kazi yake Mashariki ya Kati ilikuwa pana mno. Hakuweza kudokeza viegezo madhubuti kupanua uhuru wa Wapalestina kusafiri mji wa Gaza na maeneo yaliyokaliwa na Israel.