×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download Now

Washikadau wa sekta ya elimu kufanya mkutano kuhusu maandalizi ya mitihani

Zikiwa zimesalia takribani siku kumi na saba kabla ya kuanza kwa mitihani ya kitaifa, washikadau wa sekta ya elimu kesho watafanya mkutano kujadili namna ya kuzuia udanganyifu katika mitihani hiyo, hasa ile ya Kidato cha Nne KCSE. Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Elimu Amina Mohammed na utahudhuriwa na zaidi ya maafisa elfu moja.

Maafisa wanaotarajiwa katika mkutano huo ni manaibu kamishna wa Kaunti, ambao pia watapokezwa vifunguo vya makonteina mia nne hamsini na tisa yanayohifadhi karatasi za mitihani katika sehemu mbalimbali nchini. Maafisa hao pekee ndio wanaojukumiwa kufungua kontena hizo na kuzifunga wakati mitihani hiyo itakapoanza.

Get Full Access for Ksh299/Week
Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in

Related Topics

Elimu Mitihani