Zikiwa zimesalia takribani siku kumi na saba kabla ya kuanza kwa mitihani ya kitaifa, washikadau wa sekta ya elimu kesho watafanya mkutano kujadili namna ya kuzuia udanganyifu katika mitihani hiyo, hasa ile ya Kidato cha Nne KCSE. Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Elimu Amina Mohammed na utahudhuriwa na zaidi ya maafisa elfu moja.
Maafisa wanaotarajiwa katika mkutano huo ni manaibu kamishna wa Kaunti, ambao pia watapokezwa vifunguo vya makonteina mia nne hamsini na tisa yanayohifadhi karatasi za mitihani katika sehemu mbalimbali nchini. Maafisa hao pekee ndio wanaojukumiwa kufungua kontena hizo na kuzifunga wakati mitihani hiyo itakapoanza.