Kampuni ya Procter &Gamble inayotengeneza vitambaa vya hedhi aina ya Always, imeanza shughuli kuwasabbazia wasichana elfu 10,896 vitambaa hivyo katika maeneo mbalimbali nchini.
Chini ya mpango kwa jina “Always Keeping Girls in Schools” wasichana hao watapewa vitambaa vitakavyodumu kwa mwaka mmoja. Vilevile watapewa nguo za ndani na mafunzo kuhusu kubalekhe na ujuzi wa masuala mbalimbali ya maisha.