Wauguzi warejea kazini baada ya kuusitisha mgomo wao
Na Mate Tongola
NAIROBI, KENYA, Athari za mgomo wa Madaktari nchini zinatarajiwa kupunguwa kwa kiwango fulani, baada ya wauguzi kuusitisha mgomo wao Jumatano na kukubali kurejea kazini.
Mgomo wa wauguzi hao ulisitishwa jana alasiri baada ya wao kutia sahini makubaliano kati yao na serikali za kaunti 47 nchini ambazo zimekubali kuutambua muungano wao.
Aidha, Muungano huo chini ya Katibu Mkuu Seth Panyako umekubali nyongeza ya mishahara iliyotolewa na serikali Jumapili iliyopita.
Baadhi ya maafikiano hayo ni kuwa, wauguzi walio katika daraja la G hadi L watapata marupurupu ya shilingi elfu ishirini na walio katika daraja la M na zaidi, watapata marupurupu ya shilingi elfu kumi na tano kila mwezi.
Nyongeza hiyo itatolewa kwa awamu mbili ya asilimia 60 mwezi Januari mwaka ujao na asilimia 40 mwezi Julai.