Wauguzi warejea kazini baada ya kuusitisha mgomo wao

News
By | Dec 15, 2016

Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, Athari za mgomo wa Madaktari nchini zinatarajiwa kupunguwa kwa kiwango fulani, baada ya wauguzi kuusitisha mgomo wao Jumatano na kukubali kurejea kazini.

Mgomo wa wauguzi hao ulisitishwa jana alasiri baada ya wao kutia sahini makubaliano kati yao na serikali za kaunti 47 nchini ambazo zimekubali kuutambua muungano wao.

Aidha, Muungano huo chini ya Katibu Mkuu Seth Panyako umekubali nyongeza ya mishahara iliyotolewa na serikali Jumapili iliyopita.

Baadhi ya maafikiano hayo ni kuwa, wauguzi walio katika daraja la G hadi L watapata marupurupu ya shilingi elfu ishirini na walio katika daraja la M na zaidi, watapata marupurupu ya shilingi elfu kumi na tano kila mwezi.

Nyongeza hiyo itatolewa kwa awamu mbili ya asilimia 60 mwezi Januari mwaka ujao na asilimia 40 mwezi Julai.

Share this story
Relentless Man City keep pressure on Arsenal in Premier League title race
City are a point behind Arsenal but with a game in hand.
Kenyans clubs spike their way to knockout stage in Egypt
Kenya Pipeline qualifies for quarterfinals in Africa Club Championships.
Ladak fires 71 nett to win Kerrs memorial tourney at Vet Labs
Hiral Shah, playing off handicap 13, was the Best Sponsor prize winner with a 72 nett.
Arsenal survive Spurs fightback to boost title charge
A five-goal thriller win lifted Arsenal to four points clear at the top.
.
RECOMMENDED NEWS