Wanafunzi wateuliwa kujiunga na shule za upili

News
By | Dec 13, 2016

Na Beatrice Maganga

Waziri wa Elimu, Dkt. Fred Matiang'i amezindua rasmi shughuli ya kuyaweka wazi majina ya wanafunzi walioteuliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule mbalimbali nchini.  Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Matiang'i amesema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha madarasa yanaongezwa katika baadhi ya shule ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa. Amesema tayari mpango huo umetengewa fedha katika bajeti ya ziada ili kuufanikisha.

Na huku wanafunzi watakaoteuliwa wakitarajiwa kuanza kujiunga na shule za upili kuanzia Januari tisa, Matiang'i amewaonya walimu wakuu dhidi ya kuwaagiza wanafunzi kununua vifaa vya shule katika maduka fulani. Anasema baadhi ya walimu hao wakuu hushirikiana na wafanyabiashara kuwapunja wazazi kwa kuwauzia bidhaa kwa bei za juu mno ili wapewe asilimia fulani ya faida.

Wanafunzi wote waliopata alama mia nne na zaidi katika Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane, KCPE wameteuliwa kujiunga na shule za kitaifa nchini.

Wazazi na wanafunzi wameshauriwa kutembelea tovuti ya www.education.go.ke kupata barua za uteuzi wa wanafunzi hao. Aidha wanaweza kutuma  nambari ya usajili kwa nambari 20042.

Share this story
Thunder plot Equity Bank raid as Premier League tips off
The bankers will take on ANU Wolfpacks in their second encounter on Sunday.
Future Boxing Championships offer Kenyan boxers lessons
What it means for Kenyan teams’ participation in the inaugural Future’s Boxing Championships in Thailand.
Why Faith Kipyegon is making waves after winning 10km debut
Kipyegon, who is nicknamed the smiling assassin, is following in the footsteps of her training mates, among them two-time Olympic champion Eliud Kipchoge.
Recall times of Shikanda, Stars' diminutive defender
On May 26, 2007, Kenya, then coached by Jacob Ghost Mulee, played Nigeria in an international friendly match at Kasarani.
Kenya Army, KPA and Equity win as league second leg gets underway
Kenya Army launched their 2025-2026 KVF Men’s National League campaign with a 3-1 win against the NYS, as the second leg served off yesterday at Kasarani Indoor Arena.
.
RECOMMENDED NEWS