Wanafunzi wateuliwa kujiunga na shule za upili

News
By | Dec 13, 2016

Na Beatrice Maganga

Waziri wa Elimu, Dkt. Fred Matiang'i amezindua rasmi shughuli ya kuyaweka wazi majina ya wanafunzi walioteuliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule mbalimbali nchini.  Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Matiang'i amesema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha madarasa yanaongezwa katika baadhi ya shule ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa. Amesema tayari mpango huo umetengewa fedha katika bajeti ya ziada ili kuufanikisha.

Na huku wanafunzi watakaoteuliwa wakitarajiwa kuanza kujiunga na shule za upili kuanzia Januari tisa, Matiang'i amewaonya walimu wakuu dhidi ya kuwaagiza wanafunzi kununua vifaa vya shule katika maduka fulani. Anasema baadhi ya walimu hao wakuu hushirikiana na wafanyabiashara kuwapunja wazazi kwa kuwauzia bidhaa kwa bei za juu mno ili wapewe asilimia fulani ya faida.

Wanafunzi wote waliopata alama mia nne na zaidi katika Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane, KCPE wameteuliwa kujiunga na shule za kitaifa nchini.

Wazazi na wanafunzi wameshauriwa kutembelea tovuti ya www.education.go.ke kupata barua za uteuzi wa wanafunzi hao. Aidha wanaweza kutuma  nambari ya usajili kwa nambari 20042.

Share this story
Sevilla coach Almeyda banned for seven games after clash with referee
Sevilla coach Matias Almeyda has been banned for seven matches after his red card last weekend during a La Liga draw with Alaves.
All World Cup matches sold out, says FIFA's Infantino
All 104 matches of the 2026 World Cup will be "sold out," FIFA president Gianni Infantino says, even though tickets are still available ahead of the June 11 kickoff.
Bodo-Glimt stun Inter, Gordon hits four in Newcastle Champions League romp
Norway's Bodo/Glimt stunned Inter Milan in the Champions League, beating last season's runners-up 3-1 in the first leg of their knockout phase play-off tie
Kenyan esports star Kappa lands a professional deal in Morocco
The top two players in eBotola League will earn direct qualification to the Esports World Cup in Riyadh, Saudi Arabia, scheduled for July 2026.
Arteta urges Arsenal to 'stand up' after title bid rocked by Wolves draw
Mikel Arteta admitted Arsenal deserve criticism for the self-inflicted wounds that threaten to ruin their Premier League title bid after the leaders blew a two-goal lead
.
RECOMMENDED NEWS