Wanafunzi wateuliwa kujiunga na shule za upili

News
By | Dec 13, 2016

Na Beatrice Maganga

Waziri wa Elimu, Dkt. Fred Matiang'i amezindua rasmi shughuli ya kuyaweka wazi majina ya wanafunzi walioteuliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule mbalimbali nchini.  Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Matiang'i amesema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha madarasa yanaongezwa katika baadhi ya shule ili kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa. Amesema tayari mpango huo umetengewa fedha katika bajeti ya ziada ili kuufanikisha.

Na huku wanafunzi watakaoteuliwa wakitarajiwa kuanza kujiunga na shule za upili kuanzia Januari tisa, Matiang'i amewaonya walimu wakuu dhidi ya kuwaagiza wanafunzi kununua vifaa vya shule katika maduka fulani. Anasema baadhi ya walimu hao wakuu hushirikiana na wafanyabiashara kuwapunja wazazi kwa kuwauzia bidhaa kwa bei za juu mno ili wapewe asilimia fulani ya faida.

Wanafunzi wote waliopata alama mia nne na zaidi katika Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane, KCPE wameteuliwa kujiunga na shule za kitaifa nchini.

Wazazi na wanafunzi wameshauriwa kutembelea tovuti ya www.education.go.ke kupata barua za uteuzi wa wanafunzi hao. Aidha wanaweza kutuma  nambari ya usajili kwa nambari 20042.

Share this story
Junior Starlets gear up for World Cup qualifier encounter against Uganda
Junior Starlets have set their sights on a crucial away win over Uganda’s Teen Cranes as they aim to secure their return to the global stage.
Under-20 talents to face off in battle for tickets to world event in Eugene
The World Under-20 Championships is set for August 5-9 in Eugene.
Over 2,500 players to battle it out in Duracoat Golf Masters Series
The Duracoat Golf Masters series 2026 will be played at 12 venues before the grand finale that will be staged at Mount Kipipiri at the end of the year. 
Sh11 B more to beat AFCON 2027 deadline
Kenya requires an additional Sh11.02 billion from the Exchequer to  complete key stadiums earmarked for the 2027 Africa Cup of Nations (AFCON),
Universities raise the bar in KUSF games
The just concluded Kenya Universities Sports Federation (KUSF) Nairobi North Conference League has once again revealed the growing competitiveness of university sports in Kenya.
.
RECOMMENDED NEWS