Serikali kuchunguza kilichosababisha ajali eneo la Naivasha

News
By | Dec 12, 2016

Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, Wakenya wametakiwa kusalia watulivu huku serikali ikiendeleza uchunguzi wa mkasa wa juzi eneo la Naivasha ambapo watu arubaini waliaga dunia baada ya gari lililobeba kemikali kusababisha ajali.

Waziri wa Masuala ya Ndani mwa Taifa Joseph Nkaissery amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa gari hilo aina ya Canter lilikuwa likisafirisha kemikali hiyo kuelekea Uganda kabla ya kukosa mwelekeo karibu na soko la Kinungi, Naivasha na kuyagonga magari mengine 14.

Tayari miili ya waliofariki imesafirishwa hadi hifadhi ya maiti ya Chiromo, Nairobi huku shughuli ya kuitambua miili hiyo ikiwa imeshika kasi.

Miongoni mwa walioaga dunia na maafisa kumi na moja wa GSU ambao walikuwa wametoa huduma za ulinzi kwa Rais Uhuru Kenyatta ambaye alikuwa ziarani eneo la Bomet.

Naibu wa Rais William Ruto ni miongoni mwa waliotuma rambirambi kwa waliowapoteza wapendwa wao kwenye ajali hiyo.

Wakati uo huo, Rais Uhuru Kenyatta ameahirisha ziara yake katika kaunti ya Narok iliyotarajiwa kuanza Jumanne kufuatia ajali iliyotokea katika eneo la Karai kaunti ndogo ya Naivasha.

Katika ujumbe msemaji wa Ikulu Manoa Esipisu amesema rais atatumia mda huo kuzitembelea na kuzifariji familia za mafisa kumi na mmoja wa kikosi cha GSU kitengo cha kuwalinda watu maarufu ambao ni miongoni mwa watu 40 waliofariki dunia wakati wa ajali hiyo.

Share this story
Kenya basks in 10,000m glory at African Senior Athletics event
Diana Wanza made it a 10,000m double gold for the country when she oozed class in the women’s 25-lap contest on Friday evening.
Stage set for World U20 Champs trials
The World Under-20 Championships are scheduled for August 2–9, 2026, in Eugene, Oregon, USA.
Ingo derby now a huge test for AFC Leopards' title credentials
Leopards to pile pressure on Gor with a win against Homeboyz.
Okong'o leads experienced boxers into finals
Africa Boxing Championships middleweight champion Edwin Okong’o stormed into the finals in the first leg of the National Boxing League in Nakuru yesterday.
Senators raise questions over Sh45.8 billion Talanta Sports City Stadium project again
Sports CS Mvurya and PS Mwangi are at pains to explain the sudden increase in construction costs.
.
RECOMMENDED NEWS