Serikali kuchunguza kilichosababisha ajali eneo la Naivasha

News
By | Dec 12, 2016

Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, Wakenya wametakiwa kusalia watulivu huku serikali ikiendeleza uchunguzi wa mkasa wa juzi eneo la Naivasha ambapo watu arubaini waliaga dunia baada ya gari lililobeba kemikali kusababisha ajali.

Waziri wa Masuala ya Ndani mwa Taifa Joseph Nkaissery amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa gari hilo aina ya Canter lilikuwa likisafirisha kemikali hiyo kuelekea Uganda kabla ya kukosa mwelekeo karibu na soko la Kinungi, Naivasha na kuyagonga magari mengine 14.

Tayari miili ya waliofariki imesafirishwa hadi hifadhi ya maiti ya Chiromo, Nairobi huku shughuli ya kuitambua miili hiyo ikiwa imeshika kasi.

Miongoni mwa walioaga dunia na maafisa kumi na moja wa GSU ambao walikuwa wametoa huduma za ulinzi kwa Rais Uhuru Kenyatta ambaye alikuwa ziarani eneo la Bomet.

Naibu wa Rais William Ruto ni miongoni mwa waliotuma rambirambi kwa waliowapoteza wapendwa wao kwenye ajali hiyo.

Wakati uo huo, Rais Uhuru Kenyatta ameahirisha ziara yake katika kaunti ya Narok iliyotarajiwa kuanza Jumanne kufuatia ajali iliyotokea katika eneo la Karai kaunti ndogo ya Naivasha.

Katika ujumbe msemaji wa Ikulu Manoa Esipisu amesema rais atatumia mda huo kuzitembelea na kuzifariji familia za mafisa kumi na mmoja wa kikosi cha GSU kitengo cha kuwalinda watu maarufu ambao ni miongoni mwa watu 40 waliofariki dunia wakati wa ajali hiyo.

Share this story
Kirimi powers to glory at VetLab Club event
Ericv Karimi is the overall winner of the eighth and final leg of the Kengen golf tournament series. 
Strathmore Swords bounce back to slice Eldonets in league battle
Strathmore University Swords bounced back from Saturday’s defeat to edge out Eldonets 67-64 in a Kenya Basketball Federation (KBF) Women’s Premier League match on Sunday.
K'Ogalo silence Muranga Seal to move one win away from title
Record league champions Gor Mahia moved to within one win of another league title after beating Murang’a Seal 3-1 in a crucial SportPesa Premier League match on Sunday.
African stars in Europe: Antoine Semenyo wins it for City
Antoine Semenyo produced one of the great FA Cup final goals with an audacious back-flick that sealed a 1-0 win for Manchester City over Chelsea in the FA Cup final at the weekend.
Mixed results for top boxers as Police, KDF lead after first leg
Defending champions Kenya Police and Kenya Defence Forces shared the lead after the opening leg of the National Boxing League in Nakuru, as several top boxers suffered surprise defeats.
.
RECOMMENDED NEWS