Nipe nikupe yaendelea kati ya Ruto na Raila

News
By Carren Papai | Jul 04, 2022

Majibizano makali yameendelea baina ya pande za Naibu wa Rais William Ruto na Raila Odinga kuhusu madai ya Ruto na wandani wake kumkosea heshima Rais Uhuru Kenyatta.

Kauli ya Ruto kwamba atabuni kitengo cha mahakama cha kuchunguza miradi iliyofanywa na Kenyatta na kumwajibisha imeendelea kuibua mjadala mkali kutoka kwa wapinzani wake wanaodai kwamba yeye ni mnafiki. 

Aidha hisia mseto zimeendelea kuchipuka kufuatia suala la hivi punde ambapo Ruto amesikika katika kanda moja iliyorekodiwa, akisema nusura amzabe kofi Kenyatta kutokana na msimamo wake baada ya ushindi wao wa mwaka wa 2017 kubatilishwa na mahakama.

Wandani wa Odinga na Kenyatta wamesema Ruto alijisababishia masaibu yake na kuwaonya Wakenya dhidi ya kumchagua.

Hata hivyo, Ruto amepuuza madai hayo akisema uongozi wake utafanya kipaumbele matakwa ya Kenyatta anapostaafu sawa na kukabili hali ya kuingiliwa kwa taasisi za serikali.

Aidha viongozi wa Kenya Kwanza wameendelea kumtetea Ruto wakimlaumu Kenyatta kwa madai ya kumtenga naibu wake licha ya kumuunga mkono.

Chimbuko la malumbano haya ni kauli ya Kenyatta kumsuta vikali Ruto, na kukashifu ahadi zake alizotoa katika manifesto, akisema alishindwa kufanya yale anayoyasema akiwa naibu wa rais.

Share this story
Victor Wanyama: The Lion of Muthurwa who roared in Europe
Across his club career, Wanyama featured in 387 matches, scoring 27 goals, and representing six senior clubs in four different countries.
Harambee Starlets upbeat ahead of Fifa series
Starlets are currently in camp preparing for the tournament that will see them play Australia, India and Malawi.
Starlets and Junior Malkia Strikers in race for Soya glory
Starlets had a remarkable year, securing a return to the continental stage and excelling in other regional competitions.
Wounded giants St Anthony's and Kamusinga seek redemption
The two giants are out to salvage their pride and restore lost glory. Kamusinga returns to the national stage after three years in the cold.
Eldoret City Marathon in race to attain World Athletics label
For the last eight years, the race that has pulled the biggest crowds to Eldoret City has maintained its unique status and stature.
.
RECOMMENDED NEWS