Nipe nikupe yaendelea kati ya Ruto na Raila

News
By Carren Papai | Jul 04, 2022

Majibizano makali yameendelea baina ya pande za Naibu wa Rais William Ruto na Raila Odinga kuhusu madai ya Ruto na wandani wake kumkosea heshima Rais Uhuru Kenyatta.

Kauli ya Ruto kwamba atabuni kitengo cha mahakama cha kuchunguza miradi iliyofanywa na Kenyatta na kumwajibisha imeendelea kuibua mjadala mkali kutoka kwa wapinzani wake wanaodai kwamba yeye ni mnafiki. 

Aidha hisia mseto zimeendelea kuchipuka kufuatia suala la hivi punde ambapo Ruto amesikika katika kanda moja iliyorekodiwa, akisema nusura amzabe kofi Kenyatta kutokana na msimamo wake baada ya ushindi wao wa mwaka wa 2017 kubatilishwa na mahakama.

Wandani wa Odinga na Kenyatta wamesema Ruto alijisababishia masaibu yake na kuwaonya Wakenya dhidi ya kumchagua.

Hata hivyo, Ruto amepuuza madai hayo akisema uongozi wake utafanya kipaumbele matakwa ya Kenyatta anapostaafu sawa na kukabili hali ya kuingiliwa kwa taasisi za serikali.

Aidha viongozi wa Kenya Kwanza wameendelea kumtetea Ruto wakimlaumu Kenyatta kwa madai ya kumtenga naibu wake licha ya kumuunga mkono.

Chimbuko la malumbano haya ni kauli ya Kenyatta kumsuta vikali Ruto, na kukashifu ahadi zake alizotoa katika manifesto, akisema alishindwa kufanya yale anayoyasema akiwa naibu wa rais.

Share this story
Star-studded line-up sets stage for tight race at kip keino classic
Top Kenyan and global athletes are bracing for a high-stakes showdown at the Kip Keino Classic set for April 24 in Nairobi, with expectations running high ahead of the evening meet.
Atletico 'ready' for Champions League success at last
Atletico Madrid coach Diego Simeone said that his team was ready to finally win the Champions League after knocking out Barcelona on Tuesday to reach the semi-finals.
Ekitike injury 'looks really bad', says concerned Slot
Slot had paired Ekitike up front alongside Alexander Isak, who was making his first start since breaking his leg in December.
Dembele sends PSG past wounded Liverpool into Champions League semis
Ousmane Dembele's double guided Paris Saint-Germain into the Champions League semi-finals as a 2-0 win over Liverpool at Anfield
Will Harambee Starlets survive Australia's onslaught?
Harambee Starlets booked their place in the final after a composed 2-0 victory over India at Nyayo Stadium on Sunday.
.
RECOMMENDED NEWS