Ruto yuko Narok kupigia debe azma yake

News
By Carren Papai | Jun 18, 2022

Mgombea wa urais wa UDA William Ruto yuko katika Kaunti ya Narok ambapo anaendeleza kampeni za Kenya Kwanza kupigia debe azma yake kuwa urais.

Ruto ameandamana na vigogo wa Kenya Kwanza Musalia Mudavadi, mwenzake wa FordKenya  Moses Wetangula miongoni mwa wengine.

Akizungumza katika eneo la Kilgoris, Ruto ameahidi kuwa uongozi wake utashughulikia matatizo ambayo yamekuwa yakiwakumba watu wa Jamii ya Maa kwa muda na kuwataka kumuunga mkono Agosti tisa.

Wandani wake Moses Wetangula, Musalia Mudavadi na Ndindi Nyoro wameendelea kumpigia debe Ruto wakisema kwamba anauwezo mkubwa wa kufanikisha mabadiliko ya uongozi nchini na kuitaka Jamii ya Maa kumuunga mkono.

Aidha wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta kukoma kujihusisha na siasa za urithi na badala yake kuwaachia Wakenya nafasi ya kumchagua kiongozi wao.

Ruto baadaye Alasiri ya leo atazuru Kiambu kupigia debe azma yake wakati ambapo mvutano unaendelea kutokota miongoni mwa wa wagombea wa ugavana wa Kiambu wanaohisi kuwa Ruto anampendelea Kimani wa Matangi wa UDA.

Tayari Moses Kuria na William Kabogo wametishiakutohudhuria mikutano ya kumpigia debe Ruto wakitaka ashughulikie malalamiko yao.

Share this story
Kisii schools upgrade sibling rivalry as they fight for rugby 15s trophy
Kisii School, Cardinal Otunga Mosocho and Nyambaria Boys will be upgrading their sibling rivalry in this year’s Lake Region Term One schools championships.
Senegal stripped of AFCON title, Morocco champions - CAF
The Confederation of African Football (CAF) have stripped Senegal of the Africa Cup of Nations (AFCON) title they won in January and declared Morocco champions.
Heavyweights Kisumu Day, Yala, and Nyakach Girls eye victories
Kisumu Day, St Mary’s Yala and Nyakach Girls will be seeking to assert their dominance in hockey, rugby and basketball.
Neymar misses out as Endrick returns to Brazil squad
Brazil coach Carlo Ancelotti said on Monday Neymar is "not 100 percent" fit so will miss two friendlies later this month as youngster Endrick returns to the squad.
Chelsea fined Sh1.8 billion historical financial breaches
Chelsea were fined £10.75 million ($14.27 million) and received a suspended one-year transfer ban on Monday in relation to historical breaches of Premier League rules.
.
RECOMMENDED NEWS