Ruto yuko Narok kupigia debe azma yake

News
By Carren Papai | Jun 18, 2022

Mgombea wa urais wa UDA William Ruto yuko katika Kaunti ya Narok ambapo anaendeleza kampeni za Kenya Kwanza kupigia debe azma yake kuwa urais.

Ruto ameandamana na vigogo wa Kenya Kwanza Musalia Mudavadi, mwenzake wa FordKenya  Moses Wetangula miongoni mwa wengine.

Akizungumza katika eneo la Kilgoris, Ruto ameahidi kuwa uongozi wake utashughulikia matatizo ambayo yamekuwa yakiwakumba watu wa Jamii ya Maa kwa muda na kuwataka kumuunga mkono Agosti tisa.

Wandani wake Moses Wetangula, Musalia Mudavadi na Ndindi Nyoro wameendelea kumpigia debe Ruto wakisema kwamba anauwezo mkubwa wa kufanikisha mabadiliko ya uongozi nchini na kuitaka Jamii ya Maa kumuunga mkono.

Aidha wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta kukoma kujihusisha na siasa za urithi na badala yake kuwaachia Wakenya nafasi ya kumchagua kiongozi wao.

Ruto baadaye Alasiri ya leo atazuru Kiambu kupigia debe azma yake wakati ambapo mvutano unaendelea kutokota miongoni mwa wa wagombea wa ugavana wa Kiambu wanaohisi kuwa Ruto anampendelea Kimani wa Matangi wa UDA.

Tayari Moses Kuria na William Kabogo wametishiakutohudhuria mikutano ya kumpigia debe Ruto wakitaka ashughulikie malalamiko yao.

Share this story
Inaugural Kenya Varsity Cup launched in a colourful Nairobi ceremony
The eight-team competition will run from April 7 to May 23 at Kasarani Annex and Ulinzi Sports Complex stadiums in Nairobi.
CS Mvurya gazettes AFCON 2027 Local Organising Committee
The government has established the Pamoja Africa Cup of Nations (AFCON) 2027 Local Organising Committee (LOC) to spearhead Kenya’s preparations for the continental football tournament.
Kenya pays Sh3.9 Billion CAF hosting fee
Kenya clears Sh3.9 billion CAF hosting fee ahead of AFCON 2027, Sports CS Mvurya says ministry upgrading match venues, training facilities and other logistics
Ghana sack coach Addo 10 weeks before World Cup
Ghana have dismissed coach Otto Addo, hours after a friendly defeat to Germany and just over 70 days until the World Cup.
Indiza and Nsanzuwera join Kibugu on Sunshine Tour
Kenya’s Dismas Indiza and Rwanda’s Celestin Nsanzuwera have earned full Sunshine Tour playing rights after finishing third and second, respectively on the Sunshine Development Tour
.
RECOMMENDED NEWS