Koome aitaka IEBC kuwahakikishia Wakenya uchaguzi huru

News
By Carren Papai | Jun 04, 2022

Jaji Mkuu Martha Koome ameitaka Tume ya Uchaguzi IEBC kushughulikia kwa haraka masuala makuu yaliyosababisha kubatilishwa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017.

Akizungumza wakati wa kikao na Chama wa Wahariri Nchi kuhusu utayarifu wa Idara ya Mahakama kushughulikia kesi za baada ya uchaguzi, Koome amesema kuwa nyingi ya masuala hayo yalihusu utendakazi wa IEBC.

Koome amesema tume hiyo inastahili kuwaeleza Wakenya namna imeweka mikakati ya kuzuia kurudiwa kwa hali iliyoshuhudiwa hasa kuhusu kusambazwa na kutangazwa kwa matokeo ya kura za urais.

Kikao hicho pia kulijadili suala la wawaniaji wenye kesi mbalimbali mahakamani  hasa baada ya IEBC kusema kuwa hawawezi kuzuiwa hadi rufaa walizowasilishwa zitakaposilikizwa na kuamuliwa. Jaji Daniel Musinga anaeleza amesisitiza umuhimu wa hilo kuzingatiwa.

Koome amesema jumla ya kesi 168 za kura ya mchujo zinasikilizwa na Mahakama ya Kutatua Migogoro ya Vyama Kisiasa, 29 zikishughulikiwa na Mahakama Kuu na moja katika Mahakama ya Juu.

Share this story
Arsenal survive Spurs fightback to boost title charge
A five-goal thriller win lifted Arsenal to four points clear at the top.
Bitok cautions KCB as they fight for continental title
The bankers defeated Association Sportiff De Bejaia of Algeria in straight sets of 25-16, 25-9 and 25-21 in their opening match.
Liverpool's Premier League title hopes suffer blow, Sheffield United relegated
Wolves deepened Luton's woes with a 2-1 win and Fulham drew 1-1 with Crystal Palace.
.
RECOMMENDED NEWS