Watu sita Wauwawa na Wanamgambo wa Al Shabaab Eneo la Elwak

News
By | Jul 01, 2016

Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, WATU sita wameuliwa na wanamgambo wa Al Shabaab kuyavamia mabasi mbili eneo la Elwak, Kaunti ya Mandera.

Shambulizi hilo limetekelezwa kati ya miji ya Wargadud na Elwak baada ya wanamgambo hao kuyamininia risasi magari hayo katika kituo cha Corner S mwendo wa saa nne asubuhi.

Kamanda wa eneo la kaskazini mashariki Mohamed Saleh amesema kuwa watu sita akiwemo polisi wa akiba waliuliwa kwenye shambulizi hilo huku wengine wakiwachwa na majeraha.

Inaarifiwa kuwa mabasi hayo yalikuwa chini ya ulinzi wa polisi yaliposhambuliwa.

Ni jana ambapo Kaimu Naibu wa Kamishna wa Mandera Mashariki Yonah Nyawir alitangaza kupigwa  marufuku kwa usafiri wa wageni wanaoingia au kuondoka kaunti hiyo kwa basi hadi mfungo wa Ramadhan uishe.

Kwa mujibu wa kamati ya Usalama ya Kaunti hiyo, wasafiri wanaotumia basi mara nyingi hushambuliwa na makundi ya kigaidi.

Share this story
Experienced Okello, Chajira named in Kenya Lionesses squad for Rugby Africa Cup
Kenya Lionesses have named an experienced squad featuring Janet Okello and Sheila Chajira for the Rugby Africa Cup as they aim to improve on their previous runner-up finish.
McCarthy set for emotional South Africa reunion after AFCON Draw
Harambee Stars coach Benni McCarthy is preparing for an emotional clash against his home country after Kenya was drawn with South Africa in the 2027 Afcon qualifiers.
Junior Starlets gear up for World Cup qualifier encounter against Uganda
Junior Starlets have set their sights on a crucial away win over Uganda’s Teen Cranes as they aim to secure their return to the global stage.
Under-20 talents to face off in battle for tickets to world event in Eugene
The World Under-20 Championships is set for August 5-9 in Eugene.
Over 2,500 players to battle it out in Duracoat Golf Masters Series
The Duracoat Golf Masters series 2026 will be played at 12 venues before the grand finale that will be staged at Mount Kipipiri at the end of the year. 
.
RECOMMENDED NEWS