Watu sita Wauwawa na Wanamgambo wa Al Shabaab Eneo la Elwak

News
By | Jul 01, 2016

Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, WATU sita wameuliwa na wanamgambo wa Al Shabaab kuyavamia mabasi mbili eneo la Elwak, Kaunti ya Mandera.

Shambulizi hilo limetekelezwa kati ya miji ya Wargadud na Elwak baada ya wanamgambo hao kuyamininia risasi magari hayo katika kituo cha Corner S mwendo wa saa nne asubuhi.

Kamanda wa eneo la kaskazini mashariki Mohamed Saleh amesema kuwa watu sita akiwemo polisi wa akiba waliuliwa kwenye shambulizi hilo huku wengine wakiwachwa na majeraha.

Inaarifiwa kuwa mabasi hayo yalikuwa chini ya ulinzi wa polisi yaliposhambuliwa.

Ni jana ambapo Kaimu Naibu wa Kamishna wa Mandera Mashariki Yonah Nyawir alitangaza kupigwa  marufuku kwa usafiri wa wageni wanaoingia au kuondoka kaunti hiyo kwa basi hadi mfungo wa Ramadhan uishe.

Kwa mujibu wa kamati ya Usalama ya Kaunti hiyo, wasafiri wanaotumia basi mara nyingi hushambuliwa na makundi ya kigaidi.

Share this story
Mutiso: From a humble life in Makueni to eyeing gold in Paris
At the Paris Olympics, the 27-year-old will be chasing Olympic glory alongside Eliud Kipchoge and Benson Kipruto.
Kenyan, Egyptian clubs renew rivalry in Africa Club Championships semis
KCB to face Zamalek as KPC to battle with Al Ahly in Cairo.
Kenya chase Paris Olympics ticket in Japan
Kenya have been drawn in Group B alongside Canada, Netherlands and Australia.
Golfers to battle for honours in Kitale
At the par-72 Nakuru Golf Club layout, over 150 golfers have confirmed their participation in the Britam Insurance golf tournament.
Kenya's Padel makes strides against Argentine opponents in exhibition match
Kenyan duo conceded the match to the Argentine counterparts with a set score of 4-6 for Kenya and 6-1, 6-4 for Argentina.
.
RECOMMENDED NEWS