Zimesalia siku mbili pekee na raia wa taifa la Uganda wanatarajia kufanya uchaguzi utakaomteua Rais wa nchi hio ambaye huenda akamtoa mamlakani Yoweri Kaguta Museveni ambaye ameshikilia wadhifa huo kwa muda wa miaka ishirini na tano. Kufikia sasa kampeini za uchaguzi zimefika kikomo na wapinzani wakuu wa uchaguzi huo ni Yoweri Museveni na Kiza Besigye ambao wametoa ahadi za kuimarisha uchumi wa taifa hilo pamoja na kuahidi kazi kwa vijana .