Swala la tohara kwa jamii ya waluo ni geni, lakini kulingana na wataalam wa kiafya, tohara imepokelewa vyema kwa mtazamo kwamba inapunguza uwezo wa kuambukizwa virusi vya ukimwi na maradhi mengine ya zinaa. Hata hivyo baadhi ya wazee wa jamii hiyo wanaiona kama hatua inayoangamiza mila na tamaduni yao ya zamani ambapo vijana waling'olewa meno.Ili kubaini mabadiliko hayo ya kitamaduni, migogoro inayoikumba na faida zake John Juma alizuzungumza na wazee, na kumhoji mratibu mkuu wa tohara mkoani humo, na kutuandalia taarifa ifuatayo. Hii ni katika sehemu ya kwanza makala ukale katika usasa.