Utata unaendelea kuzingira mfumo uliotumika kuwachagua wanafunzi kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu. Frank otieno anayo taarifa kuhusu kijana mmoja - ian shimenga, aliyeibuka wa kwanza katika shule ya booker academy mjini mumias; ambaye licha ya kupata alama mia nne thelathini na mbili, hadi sasa hajapata nafasi katika shule ya kitaifa. Je, itakuwaje akose kabisa nafasi katika shule zote za kitaifa?