Gavana wa Kajiado Dkt David Nkedianye amemsuta mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria na kumtaja kama asiye na maadili yanawafaa viongozi wenye nembo ya ‘mheshimiwa’.
Akizungumza kwenye mahojiano Jumatano asubuhi katika Radio Maisha, Nkedianye amesema kwa wakati mmoja mbunge huyo alitusi viongozi katika eneo la Isinya na kumtaka akome tabia hiyo.
“Yeye ni mheshimiwa lakini nataka akome tabia ya kutusi watu. Ikiwa huna kura mahali kama kiongozi, haimaanishi uanze kutusi watu,” alisema Nkedianye.
Bw Kuria ni miongoni mwa viongozi wa chama cha Jubilee ambao wamekuwa mstari wa mbele kumpigia debe Bw Joseph Olelenku ambaye anawania kiti cha ugavana Kajiado dhidi ya Bw Nkedianye.
Mapema katika mahojiano hayo, Gavana Nkedianye aliishtumu kamati iliyotwikwa jukumu la kuandaa hafla ya maziko ya aliyekua waziri wa usalama wa ndani Joseph Nkaissery.
READ MORE
NCCK calls on IEBC to act over rampant voter bribery
Shujaa star Amaitsa joins KCB as bankers' boost squad ahead of new campaign
Kenya wins silver to qualify for 2026 World Schools Team Chess Championship
Government to construct Sh150m Abakhayo Cultural Centre in Busia
Nkedianye amesema viongozi waliochaguliwa katika kauti ya Kajiado walikosa kupewa muda wa kuhutubu na kutoa pole kwa familia ya mwendazake jambo ambalo halikuwafurahisha wakazi wa eneo hilo.
Baadhi ya viongozi katika muungano wa NASA walinyimwa ruhusa ya kuingia katika boma la Nkaissery siku chache baada ya kifo chake.