Nancy Barasa in trouble
By Standard Digital
| Jan. 14, 2012
Katika kile kilisubiriwa kwa hamu kuona iwapo watamkinga mwenzao, idara
ya mahakama leo ilionyesha kuwa kweli hii ni kenya mpya. Baraza kuu la
idara ya mahakama JSC limependekeza kuwa naibu jaji mkuu Nancy Barasa
asimamishwe kazi, na rais kibaki aunde jopo kazi la kuchunguza mwenendo
wake kutokana na lile tukio linalodaiwa alimtisha bawabu rebecca kerubo
kwa bastola. Kiongozi wa mashtaka wa serikali keriako tobiko tayari
alikuwa ameikosoa idara ya polisi, akisema iliendesha uchunguzi wake
kiholela, na ndio maana aliirejesha faili iliowasilishwa katika afisi
yake.