Na Mike Nyagwoka
Kongamano la COMESA lililohudhuriwa na viongozi kutoka mataifa kumi na manane, limeafikia uamuzi wa kumuunga mkono Waziri wa Masuala ya Kigeni, Amina Mohamed kuwa Mwenyekiti wa AU.
Mataifa hayo vilevile yameomba uungwaji mkono kwa Yacin Elmi Bouh wa taifa la Djibouti kuwa Naibu Mwenyekiti wa AU.
Uwezekano wa Amina Mohamed kutwaa wadhifa huo unaendelea kuimarika huku Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake, William Ruto wakiendelea kumpigia debe.
Mataifa ambayo kufikia sasa yamemuunga mkono Balozi Amina ni Burundi, Comoros, DR. Congo, Djibouti, Misri, Eritrea, Ethiopia, Libya, Madagascar, Malawi, Mauritius, Rwanda, Ushelisheli, Sudan, Uswizi, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
READ MORE
Legal battle over appointment of ex-M-cheza CEO to gambling authority
Court rules Kenyans can change gender markers on official documents