Kiwanda cha kutengeneza vileo cha Keroche kinatarajiwa kufunguliwa leo hii. Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi KRA itaongoza hafla ya kukifungua kianda hicho mjini Nakuru.
Hatua hii inafuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu iliyoiagiza KRA kukifungua kiwanda hicho hadi kesi iliyowasilishwa na Afisa Mkuu Mtendaji Tabitha Karanja itakaposikilizwa na kuamuliwa.
Karanja aliwasilisha kesi mahakamani dhidi ya KRA kwa kupuuza agizo lililotolewa awali kuiruhusu keroche kuendelea na biashara.
Kiwanda hicho kilifunga tarehe 22 mwezi Mei kwa kushindwa kulipa kodi ya shilingi milioni 957 inayodaiwa na KRA.
READ MORE
Ukraine police say received over 2,000 bomb threat reports in three hours
Trump says Putin agrees to pause Kyiv strikes amid harsh cold
Kenyan who escaped Russia nurses war injuries, trauma
Africa suffers Russia's war against Ukraine as some leaders play games