Kiwanda cha kutengeneza vileo cha Keroche kinatarajiwa kufunguliwa leo hii. Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi KRA itaongoza hafla ya kukifungua kianda hicho mjini Nakuru.
Hatua hii inafuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu iliyoiagiza KRA kukifungua kiwanda hicho hadi kesi iliyowasilishwa na Afisa Mkuu Mtendaji Tabitha Karanja itakaposikilizwa na kuamuliwa.
Karanja aliwasilisha kesi mahakamani dhidi ya KRA kwa kupuuza agizo lililotolewa awali kuiruhusu keroche kuendelea na biashara.
Kiwanda hicho kilifunga tarehe 22 mwezi Mei kwa kushindwa kulipa kodi ya shilingi milioni 957 inayodaiwa na KRA.
READ MORE
Ukrainian men in Poland face legal limbo
EU, UK hit Russia with joint sanctions over cyber attacks
Ukrainian and Russian strikes kill several in both countries
Ukraine allies to gather in Paris to step up pressure on Russia