Kiwanda cha kutengeneza vileo cha Keroche kinatarajiwa kufunguliwa leo hii. Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi KRA itaongoza hafla ya kukifungua kianda hicho mjini Nakuru.
Hatua hii inafuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu iliyoiagiza KRA kukifungua kiwanda hicho hadi kesi iliyowasilishwa na Afisa Mkuu Mtendaji Tabitha Karanja itakaposikilizwa na kuamuliwa.
Karanja aliwasilisha kesi mahakamani dhidi ya KRA kwa kupuuza agizo lililotolewa awali kuiruhusu keroche kuendelea na biashara.
Kiwanda hicho kilifunga tarehe 22 mwezi Mei kwa kushindwa kulipa kodi ya shilingi milioni 957 inayodaiwa na KRA.
READ MORE
Five years of Russia-Ukraine war: Will the 'Putin consensus' among Russians hold?
Putin failed to achieve goals in Ukraine, Zelensky says on war anniversary
Moscow war against Ukraine 'triple failure for Russia': Macron
Kenya suffers Russia's exploitation in the 4th year of war against Ukraine