Chama cha Madaktari KMPDU kwenye eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa kimetishia kuitisha mgomo wa madaktari kwenye Kaunti ya Nandi baada ya Serikali ya kaunti hiyo kuchelewesha mishahara yao.
Mwenyekiti wa KMPDU kwenye eneo hilo, Dr. Darwin Ambuka amesema kwa miezi kadhaa, baadhi ya madaktari wamekuwa wakilipwa huku wengine wakikosa kupokea mishahara yao kwa wakati.
Ambuka aidha amewashutumu maafisa wakuu wa wafanyakazi katika kaunti hiyo kwa madai ya kupuuza matakwa ya chama hicho ya kuwataka kuboresha mazingira ya kazi ya madaktari.
Wakati huo huo, Ambuka ameisuta serikali ya Kaunti ya Turkana kwa madai ya kupanga kuwaajiri madaktari na wataalam wengine wa afya kwa mkataba wa kandarasi kinyume na ule wa kudumu.
Chama cha KMPDU kwenye eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa kimetishia kuitisha mgomo
By Carren Omae
| Jan. 12, 2023