Jopo la Boko Haram kusababisha maafa nchini Nigeria kaskazini kila kukicha ni jambo la kusikitisha sana. Kufaulu kwa Rais Muhammadu Buhari kwenye uchaguzi Nigeria kunatoa matarajio mapya ya kupata suluhu kwa jambo hili lililokumba nchi nzima ya Nigeria.
Linaloshangaza ni kwamba kikundi kidogo cha magaidi kama Boko Haram linaweza kusababisha maafa vile wamefanya eneo za Borno na Maiduguri. Ukinoa bongo, inaonekana bayana kwamba kunao maafisa kwenye idara za kiusalama Nigeria wanaounga mkono wanamgambo wa Boko Haram.
Jumuia ya kimataifa yakiwemo Chad, Niger na Cameroon zimetia motisha juhudi za Nigeria kuangamiza Boko Haram. Uongozi wa Bwana Buhari utapata pigo kubwa asipoweza kutatua bughdha inayosababishwa na Boko Haram. Serikali ya Bwana Jonathan ilifeili kwenye uchaguzi kwa kutowajibika kukumbana na matatizo ya Nigeria hususan janga la Boko Haram.
Itabidi Bwana Buhari anoe bongo na kuongeza maarifa jitihada zote za kidiplomasia, kijeshi na kikatiba kumaliza donda ndugu la Boko Haram kaskazini mwa Nigeria.
READ MORE
Kenya bets on dual training curriculum at workplace to fix skills gap
Ramadhan spirit inspires companies, firms, individuals to share
No home to return to for woman after 25 years in prison
Accident report reveals Wilson airport still a ticking timebomb