Viongozi wa upinzani

nawaomba kwa yakini

ajenda iwe ni amani

acheni ya uchochezi

 

za humu nchini siasa

mmejaza na mikasa

vurugu bungeni hasa

acheni ya uchochezi

 

Ughaibuni mkisafiri

zungumzeni kwa ari

nchi kuipa fahari

acheni ya uchochezi

 

Uamuzi wa mahakama

ushafanyika hadi tama

ICC sasa mambo zama

acheni ya uchochezi

 

mmejawa na hekaya

kwa vyote mwaona ubaya

nauliza hamuoni haya?

Acheni ya uchochezi

 

Shida za hapa nchini

zatuhusu sote yakini

pamoja tuyatatue kwa amani

acheni ya uchochezi

 

serikali ina dosari tosha

zaweza zote kwisha

iwapo mtashiriki kusitisha

acheni ya uchochezi

 

tunapokaribia uchaguzi

enezeni amani na mapenzi

kwa wema mpate uongozi

acheni ya uchochezi

 

kwa pamoja mjenge Kenya

na serikali mwendeleze Kenya

bila chuki na tofauti Kenya

acheni ya uchochezi

 

Jina la Kenya la thamana

tuilinde tuienzi kwa sana

ukabila na ufisadi kupigana

acheni ya uchochezi

Find more articles at: 

https://yegonemmanuel.wordpress.com/

By Ochieng Oyugi 22 mins ago
Athletics
Bednarek confident ahead of showdown with Omanyala
Athletics
Time for world beaters to show their supremacy at Kip Keino Classic
Athletics
Nowicki to use Kip Keino Classic to prepare for Olympics
By AFP 7 hrs ago
Athletics
Beijing half marathon runners stripped of medals after controversial finish