Premium

Shule kufungwa Agosti, 6 kupisha uchaguzi mkuu na zitafunguliwa Agosti, 15

Shule zote nchini zitafungwa kwa muda kuanzia tarehe 6 mwezi Agosti ili kupisha shughuli ya uchaguzi mkuu wa wiki ijayo.

Akizungumza katika Shule ya Upili ya Alliance, Waziri wa Elimu Profesa George Magoha amesema shule zitafungwa kwa siku 9 hadi Agosti tarehe 15 kwa kuwa nyingi zinatumika kama vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo amesema iwapo kutafanyika duru ya pili ya uchaguzi wa basi shule zitasalia kufungwa hadi ikamiike. Amesema maandalizi ya mitihani ya kitaifa ambayo imeratibiwa kufanyika Novemba mwaka huu yanaendelea akisema iwapo shughuli za masomo zitaathirika sana na uchaguzi mkuu, basi washikadau katika sekta ya elimu watafanya jadiliano iwapo mitihani hiyo itafanyika au itaahirishwa.

Ikumbukwe kulingana na kalena ya masomo ya mwaka huu shule zinatarajiwa tena kufungwa kati ya 17 mwezi septemba hadi tarehe 25 mwezi huo kwa kipindi cha wiki moja. Muhula wa tatu unatarajiwa kuanza Septembe 26 hadi novemba 28 ambapo zitafungwa kupisha mitihani ya kitaifa ya Darasa la nane KCPE na Kidato cha Nne KCSE.

By AFP 1 hr ago
Athletics
Beijing half marathon runners stripped of medals after controversial finish
By AFP 13 hrs ago
Football
Arsenal, Liverpool fight to keep Premier League race alive
Athletics
World hammer silver medallist Kassanavoid eyes glory at Nyayo on Saturday
Athletics
Eldoret City Marathon to have a bigger 10km fun run