Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wadogo-wadogo katika Soko la Kakamega, Harey Magero anasema kwamba tangu kuondolewa kwa marufuku ya kuwa nje, sekta ya biashara inazidi kunawiri. Magero amekiri kwamba sekta hiyo ilikuwa imeathirika pakubwa kutokana na janga la korona. Benard Lusigi amefanya mahojiano naye.