.
6th March, 2021
Chanjo dhidi ya maambukizi ya korona nchini Kenya itaanza na hospitali za umma jijini nairobi kabla ya kuratibiwa kikamilifu sehemu zingine za nchi. Kwa mujibu wa Daktari Ouma Oluga wa NMS, hospitali za Pumwani, Mbagathi na mama Lucy ndizo za kwanza kutoa chanjo kwa umma wiki ijayo Nairobi naye mwenyekiti wa baraza la magavana Martin Wambora akidokeza kuwa mkutano wa jumatano na waziri wa afya Mutahi Kagwe utaratibu jinsi chanjo hiyo itatolewa kote nchini.