13th December, 2019
<style type="text/css">p.p1 {margin: 0.0px 0.0px 0.0px 0.0px; line-height: 20.1px; font: 15.0px 'Microsoft Sans Serif'} span.Apple-tab-span {white-space:pre} </style>
Kampuni ya uchapishaji ya Spotlight Publishers imesherehekea miaka kumi tangu kuanzishwa kwake na kutathmini changamoto na ufanisi uliopo katika fani ya uandishi na uchapishaji. hafla hiyo iliyoandaliwa huko Westlands Sarit Center ilihudhuriwa na waandishi wa habari, wahariri, waandishi maarufu wa vitabu wakiwemo guru Wallah Bin Wallah, Said Ahmed Mohammed kutoka Zanzibar miongoni mwa wengine. Mgeni wa heshima Dkt. julius kipng'etich aliwashauri wachapishaji kuenda na wakati kwa kuzingatia mabadiliko kwenye uwanja wa uandishi ambao sasa unachukua mkondo wa dijitali.