.
9th December, 2019
Washukiwa wanne wamefikishwa kwenye mahakama ya Githongo kaunti ya Meru na kukana shtaka la kupiga na kuumiza George Mutura na kumsababishia madhara ya kudumu mwezi Novemba mwaka huu. Washukiwa hao ni Meshack Muthomi, Bernard Mutwiri, Alfred Mutwiri, na James Mutuma walifika mbele ya hakimu mkuu wa Githongo Susan Ndegwa. Meshack Muthomi na Bernard Mutwiri walikana shtaka hilo naye Alfred Mutwiri aliachiliwa huru kwa kukosa ushahidi. James Mutuma naye aliamuriwa kuripoti katika kituo cha polisi cha Githongo. Muathiriwa kwa jina George Mutura bado anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Meru level 5.